Shirikisho la Kimataifa la Haki za Binaadamu, limewatuhumu askari wa
usalama wa serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kuvunja haki za
binaadamu nchini humo. Shirikisho hilo limesema hayo wakati likitoa
ripoti ya uchunguzi uliofanywa kuhusiana na matukio ya tarehe 30 mwezi
Disemba mwaka jana nchini Congo. Kwa mujibu wa ripoti hiyo askari wa
usalama wa serikali ya Kinshasa, walitenda vitendo vilivyo dhidi ya haki
za binaadamu, wakati wa kukabiliana na wanamgambo wa Kikristo wafuasi
wa Askofu Paul Joseph Mukungubila Mutombo.
Taasisi hiyo ya haki za
binaadamu imesema, katika operesheni za kuyakomboa maeneo kadhaa
yaliyokuwa yametekwa na wanamgambo wa askofu huyo na licha ya kwamba
wanamgambo hao walikuwa wamebebea fimbo na miti mikononi mwao, waliuliwa
kikatili na askari hao wa serikali. Ripoti imefafanua zaidi kwamba,
katika tukio hilo watu 103 waliuawa na askari hao wa serikali ya Jamhuri
ya Kidemokrasia ya Kongo. Hata hivyo taasisi hiyo imesema kuwa wahanga
wa tukio hilo ni zaidi ya watu hao 103. Aidha imesema kuwa, baadhi ya
wanachama wa askofu Mukungubila waliotiwa mbaroni hadi sasa wanaendelea
kuadhibiwa kwa mateso makali ndani ya jela za nchi hiyo. Askofu
Mukungubila Mutombo, alitiwa mbaroni katikati ya mwezi huu huko nchini
Afrika Kusini.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)







No comments:
Post a Comment