Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, May 23, 2014

Uchaguzi wa bunge Libya kufanyika tarehe 25 Juni

Kufuatia kuongezeka ukosoaji mkubwa wa kila siku juu ya kuongezwa muda wa shughuli zake hadi mwezi Disemba mwaka huu, hatimaye Kongresi ya Taifa nchini Libya yaani bunge, limetangaza kuwa, uchaguzi wa bunge utafanyika tarehe 25 mwezi ujao. Hayo yamesemwa na Naibu wa pili wa Spika wa bunge la nchi hiyo, bwana Swaleh al-Makhzum na kuongeza kuwa, tarehe 25 Juni itakuwa siku ya kihistoria kwa Walibya. Kwa utaratibu huo Kongresi ya Taifa ya Libya imemaliza kigugumizi kuhusiana na suala zima la uchaguzi huo.
Hii ni katika hali ambayo machafuko ya kila mara ambayo yanaendelea nchini humo, yamezua maswali mengi kuhusu uwezekano wa kufanyika uchaguzi huo. Wakati huo huo Jenerali mstaafu wa nchi hiyo, Khalifa Haftar  ameituhumu serikali ya mpito ya Tripoli kwamba inawaunga mkono magaidi na kusema kuwa, mapigano dhidi ya wanamgambo wenye silaha yataendelea. Zaidi ya hayo, Muhammad Hijazi, kamanda mkuu wa jeshi la Libya amesema kuwa, jeshi la taifa limejiandaa vilivyo kuendelea na vita dhidi ya makundi yenye misimamo ya kufurutu ada, magaidi na waungaji wao mkono nchini humo.

No comments: