Duru za habari nchini Mali zinaeleza kuwa, jeshi la serikali ya nchi
hiyo limepata hasara kubwa katika mapambano yake na wanamgambo wa
kaskazini mwa nchi hiyo. Msemaji wa kundi la waasi wa Tuareg maarufu kwa
jina la 'Harakati ya Ukombozi wa Azawad,' Ag At'har amesema kuwa,
wapiganaji wa kundi hilo wamewaua askari 40 wa serikali ya Mali na
kujeruhi wengine 50 katika mapigano ya hivi karibuni, kaskazini mwa nchi
hiyo. Msemaji wa harakati hiyo ambaye anaishi huko Ouagadougou, mji
mkuu wa Burkina Faso, amedai kuwa ni wanamgambo wawili tu ndio waliouawa
katika mapigano hayo na kuongeza kuwa, mbali na askari 40 kuuawa,
askari wengine 70 wa serikali wametekwa na wapiganaji hao.
Hii ni katika
hali ambayo hapo juzi askari mmoja wa vikosi vya kulinda amani vya
Umoja wa mataifa nchini Mali, alithibitisha kutokea hasara kubwa kwa
askari wa serikali ya Bamako katika vita vyake huko kaskazini mwa Mali.
Tangu siku ya Jumamosi iliyopita, mji wa Kidal, umekuwa ukishuhudia
wimbi la mapigano ya hapa na pale kati ya pande mbili. Weledi wa mambo
wanailaumu Ufaransa kwa kuhusika na mapigano hayo, ambayo ni njia moja
wapo ya kutaka kuendelea kubakisha askari wake ndani ya ardhi ya nchi
hiyo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)







No comments:
Post a Comment