Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, July 3, 2013

Watu 7 wauawa katika maandamano Misri

Watu saba wameawa katika mapigano yaliyozuka kati ya waungaji mkono na wafuasi wa Rais Muhammad Morsi hapo jana huko Cairo mji mkuu wa Misri. Watu watatu waliuawa katika ghasia zilizojiri kati ya pande mbili hizo kwenye maeneo tofauti ya Cairo.
Huku hayo yakiripotiwa wapinzani wa Morsi jana walichoma moto makao makuu ya kundi la Ikhwanul Muslimin katika mji wa Hilwan wa kaskazini mwa Misri.
Mapema hiyo jana pia jeshi la Misri liliandaa ramani ya njia kwa lengo la kumaliza mgogoro wa kisiasa nchini humo ambapo kwa mujibu wa ramani hiyo ya njia, itabidi bunge livunjwe na katiba isimamishwe.
Wakati huo huo Rais Muhammad ameliomba jeshi la nchi hiyo kuondoa muda wake liliouainisha kwa ajili ya kusimamisha katiba na kulivunja bunge huku akiashiria juu ya uhalali wa kikatiba wa utawala wake.

No comments: