Leo ni Jumatano tarehe 24 Shaaban 1434 Hijria inayosadifiana na Julai 3, 2013.
Siku kama ya leo miaka 25 iliyopita
ndege ya abiria aina ya Airbus ya shirika la ndege ya Iran iliyokuwa
ikitoka Bandar Abbas kusini mwa Iran na kuelekea Dubai, Umoja wa Falme
za Kiarabu ilishambuliwa kwa makombora mawili kwenye maji ya Ghuba ya
Uajemi. Manowari ya kijeshi ya Marekani USS Vincennes ilifyatua
makombora hayo na kuua shahidi watu wote 298 waliokuwa katika ndege
hiyo. Shambulio hilo lilidhihirisha zaidi unyama wa serikali ya
Marekani. Viongozi wa Marekani walizidisha ukatili wao pale
walipomzawadia medali ya ushujaa nahodha wa meli hiyo kutokana na
kitendo hicho kilichoonekana na serikali ya Washington kuwa eti ni cha
kishujaa.
Siku kama ya leo miaka 43 iliyopita,
inayosadifiana na 12 Tir 1349 Hijria Shamsia, alifariki dunia Allamah
Abdul Hussein Amini, faqihi mkubwa na mwandishi hodari wa Kiislamu.
Kitabu cha kwanza cha mwanazuoni huo alikipa jina la Shuhadaul Fadhila.
Hata hivyo kitabu mashuhuri na kikubwa zaidi cha Allamah Amini ni kile
cha "al Ghadiir Fil Kitab Wassunah" ambamo ndani yake amekosoa na
kuchunguza vitabu vikubwa na marejeo vya Kiislamu 150 akithibitisha
wilaya na haki ya Imam Ali bin Abi Twalib ya kuwa Khalifa na Imam wa
Waislamu baada ya Mtume Muhammad (saw). Mwanachuoni huyo alisafiri kwa
taabu katika nchi za India, Uturuki, Syria, Misri na Iraq kwa ajili ya
kukusanya ushahidi mbalimbali wa kihistoria alioutumia katika kitabu
hicho.
Na siku kama ya leo miaka 109 iliyopita
inayosadifiana na 3 Julai 1904, alifariki dunia Theodor Herzl mwasisi wa
harakati ya Kizayuni. Herzl alizaliwa mwaka 1860 mjini Bucharest mji
mkuu wa Hungary na kisha kuelekea Austria. Mnamo mwaka 1897, aliasisi
Taasisi ya Kimataifa ya Kizayuni kwenye kongamano lililofanyika nchini
Uswisi. Herzl alifariki mwaka 1904, huku akiwa ameacha mikakati ya
kuasisiwa utawala ghasibu wa Kizayuni wa Israel, kwenye ardhi za
Palestina utawala ambao hadi leo unaendelea kufanya jinai kubwa na
kusababisha maafa yasiyo na kifani dhidi ya wananchi madhlumu wa
Palestina.







No comments:
Post a Comment