Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, July 13, 2013

Tsvangirai apinga tarehe ya uchaguzi wa rais

Wakati zimesalia siku 19 kabla ya kufanyika uchaguzi wa rais nchini Zimbabwe na huku kampeni za uchaguzi huo zikipamba moto, Morgan Tsvangirai, Waziri Mkuu wa Zimbabwe na kiongozi wa chama cha MDC ameiandikia barua Jumuiya ya Ustawi ya Kusini mwa Africa SADC akilalamikia maamuzi yaliyochukuliwa hivi karibuni na Rais Robert Mugabe wa nchi hiyo ya kufanyika uchaguzi wa rais tarehe 31 Julai mwaka huu.

Tsvangirai amesema kuwa, uchaguzi huo utakuwa si wa kisheria, huru na wa  haki  iwapo utafanyika tarehe hiyo iliyopangwa na Rais Mugabe. Naye Tendai Biti Waziri wa Fedha wa Zimbabwe na ambaye pia ni Katibu Mkuu wa chama cha MDC amesema kuwa, hadi sasa hakuna hatua zozote zilizochukuliwa za kufanyika marekebisho muhimu nchini humo.
Hivi karibuni wakuu wa SADC walikutana kwenye kikao cha dharura huko Maputo mji mkuu wa Msumbiji, na kumtaka Rais Mugabe aakhirishe tarehe ya uchaguzi iliyopangwa awali kwa wiki mbili zaidi, mapendekezo ambayo yalipuuzwa na Rais Mugabe. Chama cha MDC kinataka yafanyike marekebisho kwenye vyombo vya habari, kikosi cha usalama na jeshi la polisi, taasisi ambazo zinadhibitiwa na Rais Mugabe wa Zimbabwe.

No comments: