Olusegun Obasanjo Rais wa zamani wa Nigeria ameteuliwa na Umoja wa
Afrika kuwa mkuu wa jopo la waangalizi wa uchaguzi mkuu nchini
Zimbabwe. Taarifa zinasema kuwa, Umoja wa Afrika umeeleza kuwa, taasisi
na asasi nyingine zisizokuwa za kiserikali na wajumbe kutoka nchi
wanachama wa Jumuiya ya Ustawi ya Kusini mwa Afrika SADC watakuwa
miongoni mwa waangalizi wa uchaguzi huo uliopangwa kufanyika tarehe 31
mwezi huu.
Uchaguzi huo unafanyika katika hali ambayo, Morgan Tsvangirai
Waziri Mkuu wa Zimbabwe na kiongozi wa chama cha MDC anadai kuwa,
vyombo vya kupasha habari, kikosi cha usalama na jeshi la polisi hivyo
vyote bado vinadhibitiwa na Rais Mugabe wa nchi hiyo. Wakati huohuo,
Umoja wa Ulaya umetangaza uwezekano wa kuondolewa vikwazo dhidi ya
Zimbabwe iwapo uchaguzi huo utakuwa huru na wa haki. Roland van de Geer
Balozi wa Umoja wa Ulaya amesema nchini Afrika Kusini kwamba, iwapo
waangalizi wa kieneo watathibitisha kuwa uchaguzi huo ulifanyika bila ya
mizengwe yoyote, umoja huo utaondoa vikwazo dhidi ya serikali ya Rais
Robert Mugabe wa nchi hiyo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)







No comments:
Post a Comment