Rais Obama wa Marekani amewasili leo nchini Tanzania ikiwa ni nchi ya
mwisho kuitembelea katika safari yake ya kuzitembelea nchi za eneo la
Kuisni mwa Jangwa la Sahara.
Obama amelakiwa mjini Dar es salaam na Rais Jakaya Kikwete wa
Tanzania, viongozi mbalimbali wa serikali pamoja na umati mkubwa wa watu
waliokuwa wakicheza, kupiga vigelegele na kupeperusha bendera za nchi
hizo mbili.
Hii ni ziara ya pili ya Rais wa Obama Barani Afrika na anaitembelea
Tanzania baada ya ziara ya Rais Xi Jimping wa China aliyeitembelea nchi
hiyo Machi 28 mwaka huu. Miongoni mwa sababu zinazoelezwa za safari ya
Obama nchini Tanzania ni nchi hiyo kuwa miongoni mwa nchi 10 duniani
ambazo uchumi wake unakua kwa kasi.







No comments:
Post a Comment