Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, July 2, 2013

Mahakama yaingilia mgomo wa walimu Kenya

Mahakama ya Viwanda nchini Kenya imetoa agizo linalowataka walimu wa shule za umma walioko mgomoni kusitisha mgomo huo na kuripoti katika maeneo yao ya kazi kesho Jumanne saa mbili asubuhi.
Agizo hilo la mahakama ya viwanda limetolewa baada ya serikali kudai kwamba mgomo wa walimu ulioanza Jumanne iliyopita si halali. Mahakama hiyo aidha imeitaka serikali kubuni kamati ya maridhiano itakayoongoza mazungumzo kati yake na chama cha walimu. Hata hivyo, mwenyekiti taifa wa chama cha walimu nchini humo KNUT, Bw. Wilson Sossion amesema walimu hawatotii agizo hilo na kusisitiza kwamba mgomo utaendelea.

Weledi wa masuala ya sheria wameonya kwamba huenda viongozi KNUT wakachukuliwa hatua za kisheria iwapo wataendelea kukaidi agizo la mahakama. Walimu wanadai marupurupu yao kulingana na mkataba wa mwaka 1997 waliotiliana saini na serikali.

No comments: