Leo ni Jumanne tarehe 23 Shaaban 1434 Hijria sawa na tarehe 2 Julai 2013.
Siku kama ya leo miaka 124 iliyopita mfumo wa kisultani ulifutwa huko
Brazil na badala yake ukaasisiwa mfumo wa jamhuri bila ya umwagaji damu
wowote na katika hali ya utulivu. Mfalme wa mwisho wa Brazil alikuwa
Pedro wa Pili ambaye alifanya jitihada za kufanya mabadiliko nchini
humo. Hatua za mfalme huyo hususan ile ya kuondoa biashara ya utumwa
mwaka 1888, iliwakasirisha wamiliki waliokuwa wakiunga mkono mfumo wake
wa kisultani. Pedro wa Pili alienguliwa madarakani bila ya mapambano
yoyote na mfumo wa jamhuri ukaasisiwa nchini Brazil.
Miaka 88 iliyopita katika siku kama hii ya leo alizaliwa Patrice
Lumumba mwasisi wa Kongo. Lumumba alitoa mchango mkubwa katika juhudi za
kukombolewa Kongo wakati wa harakati za ukombozi wa nchi za Kiafrika.
Lumumba aliteuliwa kuwa Waziri Mkuu na Waziri wa Ulinzi baada ya kuundwa
Jamhuri ya Kongo mwaka 1960. Patrice Lumumba aliuawa mwaka 1961 na
vibaraka wa Marekani na Ubelgiji baada ya kuvumilia mateso na unyama
mkubwa. Patrice Lumumba aliandika vitabu kadhaa wakati wa uhai wake na
mashuhuri zaidi ni kile alichokita" Kongo, Nchi Yangu."
Na tarehe 11 Tir miaka 31 iliyopita Ayatullah Muhamad Saduqi alimu
mkubwa, mwanamapambano na Imamu wa Ijumaa wa mji wa Yazd huko katikati
mwa Iran, aliuawa shahidi na vibaraka wa kundi la kigaidi la Munafiqiin
na kuwa shahidi wa nne aliyeuawa katika mihrabu ya swala katika historia
ya Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran. Ayatullah Muhamad Saduqi alikamilisha
masomo yake ya kidini katika Hauza ya mji mtakatifu wa Qum Iran na
kustafidi na bahari kubwa ya elimu kutoka kwa walimu mashuhuri wa kituo
hicho cha kielimu kama vile Ayatullah Burujerdi na Ayatullah Khansari.







No comments:
Post a Comment