Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail
Showing posts with label Mazungumzo ya amani Congo yasimama. Show all posts
Showing posts with label Mazungumzo ya amani Congo yasimama. Show all posts

Friday, January 25, 2013

Mazungumzo ya amani Congo yasimama, Kampala

Mazungumzo ya kusaka amani kwa ajili ya maeneo ya mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo baina ya ujumbe wa waasi wa eneo hilo na serikali ya Kinshasa yamesimamishwa.
Habari ya kusimamishwa mazungumzo hayo yaliyokuwa yakifanyika Kampala nchini Uganda imetangazwa na ujumbe wa waasi wa kundi la M23.
Mjumbe wa kundi hilo amesema kuwa mazungumzo hayo yamesimamishwa baada ya kutokuwepo maendeleo ya aina yoyote. Ameongeza kuwa kikao cha mwisho baina ya pande hizo mbili kilifanyika tarehe 18 Januari.