Maafisa wa kijeshi nchini Yemen sasa wameitaka Marekani iache
kuingilia mambo yake ya ndani. Wakizungumza Jumamosi, maafisa hao wa
kijeshi wamesema Marekani inapaswa kusitisha oparesheni zake za ndege
zisizo na rubani (drone) ambazo zinatekeleza mauaji nchini humo. Aidha
wamesema vikosi vya usalama vya Yemen ndivyo vyenye jukumu la kuwalinda
Wayemen kutokana na hujuma za kigaidi na hivyo vikosi vya kigeni
havipaswi kujihusisha na suala hilo.
Maafisa hao wameongeza kuwa
Marekani imepelekea ugaidi kuongezeka Yemen kwa kutumia ndege zisizo na
robani.
Mbali na Yemen, Marekani imekuwa ikitumia ndege hizo zisizo na rubani
kushambulia maeneo mbalimbali ya nchi za Kiislamu za Somalia,
Afghanistan, Syria na Pakistan kwa kisingizio cha kupambana na ugaidi.
Katika nchi hizo pia aghalabu ya wanaopoteza maisha katika hujuma za
ndege hizo za Marekani ni raia wa kawaida wakiwemo wanawake na watoto
wasio na hatia.







No comments:
Post a Comment