Leo ni Jumamosi tarehe 4 ya mwezi mtukufu wa Ramadhani mwaka 1434 Hijiria mwafaka na tarehe 13 Julai mwaka 2013 Miladia.
Siku kama ya leo miaka 64 iliyopita, moto mkubwa ulitokea huko Roma
mji mkuu wa utawala wa kifalme wa Rumi. Sehemu kubwa ya mji wa
kihistoria na mkongwe wa Roma iliungua na wakazi wengi wa mji huo
walipoteza maisha yao kutokana na moto huo.
Moto huo ulikuwa kisingizio
tosha kwa Nuren mtawala mmwagadamu wa Kirumi ambaye aliwauwa kwa umati
watu zaidi ya laki moja na baadaye kuwatuhumu Wakristo kuwa ndio
walioanzisha moto huo.
Miaka 858 iliyopita yaani tarehe 4 Ramadhani mwaka 576 Hijria,
alifariki dunia, Muhammad bin Muhammad mashuhuri kwa jina la Ibnu
Khorasani. Ibnu Khorasani alikuwa mshairi, mwandishi na mtaalamu wa
elimu ya Nahw. Alizaliwa mwaka 494 Hijria huko Khorasan kaskazini
mashariki mwa Iran. Akiwa na lengo la kutafuta elimu, Muhammad bin
Muhammad alielekea katika mji wa Baghdad nchini Iraq. Kutokana na kipaji
alichonacho, alimu huyu alifanikiwa kuzikwea haraka haraka daraja za
kielimu na kuondokea kuwa alimu mkubwa na mtajika.
Siku kama ya leo miaka 242 iliyopita, baharia na nahodha mashuhuri wa
Kiingereza aliyejulikana kwa jina la James Cook alikamilisha safari
yake ya kitafiti na kielimu ya kuelekea The Great Southern Continent.
Safari hiyo ilikuwa imeanza tarehe 26 Julai mwaka 1768. Safari hiyo
ndefu iliishirikisha pia timu ya watalaamu wa elimu ya Sayansi Asilia au
Natural Science kwa kimombo. Wataalamu hao walikuwa na nia ya kufanya
utafiti wa kielimu kuhusiana na mimea pamoja na viumbe wanaopatikana
katika maeneo hayo.







No comments:
Post a Comment