Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Thursday, June 20, 2013

UN yalaani kushambuliwa ofisi yake Mogadishu

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon amelaani shambulizi la waasi wa al Shabab lililolenga ofisi ya umoja huo nchini Somalia.
Msemaji wa Katibu Mkuu wa UN Martin Nesirky ameeleza kuwa, Ban Ki-moon amesema Umoja wa Mataifa haupaswi kuvunjwa moyo katika kutekeleza majukumu yake nchini Somalia na kwamba utaendelea na mipango yake ya kuwasaidia Wasomali.
Katika shambulizi hilo, al Shabab walitega bomu kwenye gari nje ya ofisi ya Umoja wa Mataifa katika mji mkuu Mogadishu ambapo watu 15 waliouawa. Miongoni mwa waliouawa ni afisa wa UNDP, makandarasi watatu kutoka Afrika Kusini na walinzi wanne wa Kisomali.
Umoja wa Mataifa hivi karibuni ulihamishia shughuli zake mjini Mogadishu kutoka nchi jirani ya Kenya, baada ya kuwa huko kwa miaka mingi kutokana na hofu ya usalama. Hii ni mara ya kwanza ofisi za Umoja wa Mataifa kushambuliwa mjini Mogadishu, tangu taasisi hiyo ilipoanza shughuli zake nchini Somalia.

No comments: