Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Thursday, June 20, 2013

Wanamgambo waua watu 72 nchini Nigeria

Watu wasiopungua 50 wameuawa na wanamgambo wenye silaha katika eneo la Zamfara nchini Nigeria. Imeripotiwa kuwa watu karibu 50 wenye silaha walizingira eneo hilo jana mapema asubuhi na kumlenga kwa risasi kila mtu mzima aliyeonekana kwenye eneo hilo. Miongoni mwa waliouawa ni imamu na kiongozi wa eneo hilo.

Wakati huo huo watu 32 wameuawa katika eneo la Maiduguri jimbo la Borno. Mauaji hayo yamefanywa na watu wanodaiwa kuwa wafuasi wa kundi la Boko Haram katika mashambulizi tofauti. Polisi imeripoti kuwa mashambulizi hayo ya kigaidi yalifanywa dhidi ya shule ya msingi na ya sekondari kwenye eneo hilo na kushambuliwa wanafunzi waliokuwa wakifanya mitihani. Tangu Mei 15 jeshi la Nigeria linajitahidi kukabiliana na wafuasi wa Boko Haram nchini humo.

No comments: