Waziri Mshauri wa Mambo ya Nje wa Ethiopia amesema kuwa, kikao
kati ya Tedros Adhanom Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo na mwenzake
wa Misri Kamel Amr kuhusiana na ujenzi uliozusha mjadala wa bwawa katika
Mto Nile kimefanyika vizuri na kwa mafanikio. Ameongeza kuwa, wanaamini
kuwa iwapo maji ya Mto Nile yatatumiwa kwa maslahi ya pande zote,
yanaweza kukidhi mahitaji ya nchi zote zilizoko pambizoni mwa mto huo na
kubaki.
Hatua ya Ethiopia ya kuamua kujenga bwawa kubwa katika Blue Nile ili
kuzalisha umeme imezusha mvutano na Misri ambayo inahofia kuwa ujenzi
huo utapunguza fungu lake la maji ya Mto Nile.







No comments:
Post a Comment