Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, June 8, 2013

'Ujumbe wa Mtume ulikuwa ni kuwaokoa watu wote'

Rais Mahmoud Ahmadinejad wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa ujumbe wa Mtume Mtukufu SAW ulikuwa ni kuwaokoa walimwengu wote. Akizungumza mbele ya viongozi wa mfumo wa Kiislamu, mabalozi wa nchi za Kiislamu walioko Tehran kwenye Husseiniya ya Imam Khomeini MA, Rais Ahmadinejad amesema kuwa, ujumbe mkuu wa Mtume SAW ulikuwa ni kumuongoza mwanadamu na shakhsia huyo aliweza kukabiliana na vikwazo mbalimbali katika kufanikisha ujumbe huo. Katika sehemu nyingine ya  hotuba yake, Rais Ahmadnejad amesema kuwa, mapinduzi ya Kiislamu ya Iran yaliyoongozwa na Imam Khomeini MA, yalikuwa yakiwalingania watu kufuata njia ya saada ya Mtume wa Mwenyezi Mungu na kusisitiza kuwa, uadilifu kamili upatatikana baada ya kudhihiri Imam wa Zama 'Mwenyezi Mungu aharakishe kudhihiri kwake.'

No comments: