Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, June 8, 2013

Magaidi 11 hatari watiwa mbaroni nchini Iraq

Jeshi la Iraq limetangaza kuwa, limefanikiwa kuwatia mbaroni magaidi 11 ambao walikuwa wakitafutwa kwa muda mrefu, kwa kuhusika na vitendo vya kigaidi huko kaskazini mwa nchi hiyo. Jeshi la usalama limetangaza kuwa, magaidi hao walitiwa mbaroni katika oparesheni kali iliyofanyika mjini Mosul katikati ya mkoa wa Nainawah kaskazini mwa Iraq. Limeongeza kuwa, mbali na magaidi hao, jeshi pia limefanikiwa kudhibiti silaha na zana nyingine za kijeshi za magaidi hao. Aidha hapo jana vilifanikiwa kugundua gari lililokuwa limetegwa bomu tayari kulipuliwa huko kusini mwa mji wa Mosul na kumtia mbaroni mtu mmoja. Wakati huo huo raia 14 waliuawa na kujeruhiwa hapo jana katika miripuko miwili iliyotokea katika eneo la Nahrawan mjini Baghdad. Kabla ya hapo pia mabasi mawili ya wafanyaziara wa Kiirani yalilipuliwa kwa mabomu nchini humo na kusababisha mauaji na majeruhi.

No comments: