Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, June 7, 2013

Serikali ya Brazzaville yasisitizia kufanyika uchaguzi

Kwa mara nyingine serikali ya Congo Brazzaville, imesisitizia udharura wa kufanyika uchaguzi wa serikali za mitaa. Hayo yalisemwa jana usiku na mwakilishi wa serikali ya Congo Brazzaville ambaye alitabiri kufanyika uchaguzi huo mwezi Julai mwaka huu. Séraphin Ondélé ambaye pia ni moja ya maafisa wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi hiyo aliyasema hayo katika ufunguzi wa kikao cha wanaharakati wa jumuiya za kiraia kilichofanyika kwa lengo la kuandaa mazingira ya kufanyika uchaguzi huo na kutekeleza maoni ya wapiga kura nchini humo. Kikao hicho kilifadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Kimataifa PNUD. Itakubukwa kuwa, uchaguzi huo uliakhirishwa, katika mazungumzo ya kisiasa yaliyofanyika tarehe 23 hadi26 mwezi Machi mwaka huu, mjini Dolisie, moja ya miji muhimu ya Congo Brazzaville.

No comments: