Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, June 7, 2013

Maachafuko yaendelea kaskazini mwa Mali

Harakati ya Kitaifa ya Ukombozi ya Azawad ambayo ni moja ya makundi ya upinzani nchini Mali, imetangaza kuwa, haitonyamazia kimya shambulizi lolote la majeshi ya nchi hiyo kama ambavyo pia haitokubali kuweka chini silaha. Harakati hiyo imesisitiza kuwa, wapiganaji wake hawatoweka chini silaha zao na wala kunyamazia kimya mashambulizi ya askari wa serikali dhidi ya maeneo ya mji wa Anefis, wa kusini mwa jimbo la Kidal, kaskazini mwa Mali. Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Mossa Ag Attaher, Msemaji wa harakati hiyo amesisitiza kuwa, Harakati ya Kitaifa ya Ukombozi ya Azawad, haitaweka chini silaha zake maadamu hali ya usalama haijarejea katika maeneno ya kaskazini mwa Mali. Ni vyema kukumbusha kuwa, viongozi wa serikali ya Bamako na wawakilishi wa harakati hiyo wanatazamiwa kukaa kwenye meza moja ya mazungumzo mjini Ouagadougou, Burkina Faso  kwa lengo la kujadili mgogoro wa nchi hiyo

No comments: