Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Thursday, June 20, 2013

Idadi ya waliouawa Mogadishu yaongezeka

Idadi ya wahanga wa shambulizi lililotekelezwa na kundi la Ash-Shabab mjini Mogadishu Somalia, dhidi ya ofisi ya Umoja wa Mataifa, imeongezeka na kufikia watu 18.
Duru za habari kutoka hospitali ya Somalia zimearifu kuwa, idadi ya wahanga wa shambulio hilo imeongezeka na kufikia watu 18 baada ya kufariki dunia raia wengine watatu mapema leo. Kwa mujibu wa ripoti hiyo wahanga wanne wa shambulizi hilo lililotokea jana ni raia wa kigeni huku wengine saba wakiwa raia wa Somalia.

Baada ya shambulizi hilo askari wa Umoja wa Afrika kwa kushirikiana na wale wa Somalia, walifanikiwa kudhibiti jengo hilo la Umoja wa Mataifa ambalo lilikuwa limedhibitiwa na wanamgambo wa Ash-Shabab na kuwaua saba kati yao.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon amelaani shambulizi la waasi wa al Shabab lililolenga ofisi ya umoja huo nchini Somalia. Hivi karibuni Umoja wa Mataifa ulihamishia shughuli zake mjini Mogadishu kutoka nchi jirani ya Kenya, baada ya kuwa huko kwa miaka mingi kutokana na hofu ya usalama.

No comments: