Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Thursday, June 20, 2013

"Fatwa za kupambana na askari wa Syria zikomeshwe"

Naibu Katibu Mkuu wa Harakati ya Kiislamu ya an-Nahdha ya Tunisia amekosoa vikali fatwa za Yusuf Qardhawi, Mkuu wa Umoja wa Maulama wa Kiislamu za kuhalalisha vita dhidi ya jeshi la Syria.
Abdelfattah Mourou amekosoa vikali fatwa hizo na kusema kuwa, Sheikh Qardhawi amekosea vikali kutoa fatwa ya kuhalalisha vita dhidi ya utawala wa Rais Bashar al-Assad wa Syria na kwamba, hazina mashiko yoyote katika misingi ya dini ya Kiislamu.
Aidha Naibu Katibu Mkuu wa Harakati ya an-Nahdha ya Tunisia, amesisitizia udharura wa kukomeshwa fatwa kama hizo huku akimtaka Qardhawi kurejea kwenye misingi asili ya dini tukufu ya Kiislamu. Sheikh Abdelfattah Mourou amewataka mashekhe wengine wanaotoa fatwa mbaya kama hizo wabadilishe mienendo yao ili kusitisha umwagaji damu wa Waislamu wenzao huko nchini Syria.
Hivi karibuni Chuo Kikuu cha al Azhar nchini Misri, kilitoa tamko la maulama wa kidini akiwemo Yusuf Qardhawi mwenyewe, kikipinga wito wa kile kinachosemwa eti ni jihadi nchini Syria na kwamba, chuo hicho hakijawahi kuunga mkono wala kutia saini wito huo.

No comments: