Waziri Mkuu mpya wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina, Rami Hamdallah
amemkabidhi Rais wa mamlaka hiyo, Mahmoud Abbas barua ya kujiuzulu
kutokana na kile kinachotajwa kuwa mkwaruzano kati yake na manaibu wake
wawili.
Hatua hiyo ya Hamdallah imewashangaza wengi kwani hajamaliza hata
majuma mawili tangu alipoapishwa. Duru za karibu na msomi huyo zinaarifu
kuwa, manaibu wake wawili wamekuwa wakihujumu juhudi zake za kuunda
serikali ya umoja wa kitaifa huko Palestina.
Rami Hamdallah aliteuliwa kuchukua nafasi ya mtangulizi wake, Salam
Fayadh aliyejiuzulu mwezi Aprili. Haijabainika iwapo Mahmoud Abbas
amekubali barua hiyo ya kujiuzulu au la.
Kabla ya kuteuliwa kuwa Waziri Mkuu, Rami Hamdallah alikuwa mkuu wa
Chuo Kikuu cha al-Najah kilichoko katika eneo la Ukingo wa Magharibi mwa
Mto Jordan katika ardhi za Wapalestina zinazokaliwa kwa mabavu na
Wazayuni.







No comments:
Post a Comment