Baraza la Mpito katika Jamhuri ya Afrika ya Kati limemuidhinisha
kiongozi wa kundi la SELEKA, Michael Djotodia kuwa rais wa mpito wa nchi
hiyo. Baraza hilo lenye wanachama 105 limemuidhinisha baada ya
kukosekana mpinzani. Mwezi uliopita, Djotodia aliwaongoza waasi wa
SELEKA kuipindua serikali ya Rais Francois Bozize ambaye kwa sasa
anaishi uhamishoni nchini Benin.
Umoja wa Afrika pamoja na taasisi
zingine za kimataifa zilikataa kumtambua kiongozi huyo wa waasi na
badala yake akatakiwa kuunda baraza la mpito litakalokuwa na jukumu la
kuandaa uchaguzi mkuu baada ya mwaka mmoja. Haijabainika iwapo jamii ya
kimataifa itamtambua Djotodia baada ya kuidhinishwa rasmi na baraza hilo
la mpito au la. Punde baada ya kuidhinishwa, kiongozi huyo wa SELEKA
ameahidi kwamba hatogombea urais wakati wa uchaguzi mkuu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)







No comments:
Post a Comment