Askari wamepambana na wafungwa waliosusia chakula katika jela ya kuogofya ya Jeshi la Marekani ya Guantanamo Bay, Cuba.
Taarifa rasmi zinasema ghasia ziliibuka pale wanajeshi wa Marekani
walipojaribu kuwapelekea wafungwa katika seli binafsi kila moja.
Mawakili wanaowatetea wafungwa katika jela ya Guantanamo huko Cuba
inayosimamiwa na Marekani wamesema kuwa baadhi ya wafungwa waliogoma
kula chakula wataaga dunia iwapo wataendelea kususia chakula.
Mawakili
hao wamesema kuwa wanasikitishwa na hali mbaya za wafungwa hao walioanza
mgomo wa kutokula chakula Februari 6 mwaka huu. Wamesema pia kwamba
wafungwa wengi waliogoma kula wamepungua sana uzito wa mwili na kwamba
sasa wanalishwa kwa nguvu kupitia puani. Watetetezi wa haki za binadamu
jana walifanya maandamano makubwa katika miji zaidi ya 26 na majimbo 19
ya Marekani katika kuadhimisha "Siku ya Kuchukua Hatua ya Kuifunga Jela
ya Guantanamo na Kuhitimisha Kuwashikilia Washukukiwa Kusiko na Mwisho."






No comments:
Post a Comment