Chuki dhidi ya Waislamu nchini Ufaransa zinazidi kuongezeka baada ya
makaburi ya Waislamu kushambuliwa na makundi yenye misimimamo ya
kupindukia mpaka. Taarifa zinasema kwamba, watu wanaodhaniwa kuwa
wafuasi wa fikra za kufurutu ada na ambao wana chuki na Uislamu
wameyashambulia makaburi ya Waislamu katika eneo la Aisne nchini humo.
Makaburi yapatayo 70 hadi 100 yameharibiwa katika shambulio hilo la
chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu nchini Ufaransa.
Uchunguzi
kuhusiana na tukio hilo umeanza kufanywa na polisi ya nchi hiyo. Wafuasi
wa makundi na vyama vya kufurutu ada nchini Ufaransa ni miongoni mwa
wafuasi wa mrengo wenye misimamo ya utaifa ambao kikawaida ndio ambao
huhusika na vitendo kama hivi. Utafiti uliofanywa unaonyesha kuwa,
vitendo vya chuki dhidi ya Uislamu na Waisalamu nchini Ufaransa
vimeongezeka mno katika siku za karibuni.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)







No comments:
Post a Comment