Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, February 24, 2012

Mahakama ya ICC yatoa kibali cha kufanyika uchunguzi Ivory Coast

Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) imetoa kibali cha kufanyika uchunguzi kuhusu mapigano ya umwagaji damu yaliyotokea miaka kadhaa iliyopita nchini Ivory Coast.
Mahakama ya ICC imetangaza kuwa majaji wa mahakama hiyo wametoa kibali kipya cha kufanyika uchunguzi kuhusu mauaji ya Ivory Coast. Kibali hicho kinampa Mwendesha Mashtaka wa ICC haki ya kufanya uchunguzi nchini Ivory Coast kuhusu jinai dhidi ya binadamu na jinai za kivita zilizofanyika nchini humo baada ya mwaka 2002.

Kutolewa kibali hicho huenda kukapelekea kutiwa mbaroni watuhumiwa wengine wa mauaji na machafuko ya Ivory Coast hususan wafuasi wa Rais wa sasa wa nchi hiyo Alassane Ouattara.
Awali Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ilikuwa imetoa kibali cha kufanyika uchunguzi kuhusu jinai ziliofanyika baada ya tarehe 28 Novemba mwaka 2010 na matukio yaliyofuatia uamuzi wa rais wa zamani wa Ivory Coast Laurent Gbagbo wa kukataa kukabidhi madaraka ya nchi kwa rais mpya wa nchi hiyo. Zaidi ya watu elfu tatu waliuawa na malaki ya wengine kukimbia makazi yao katika machafuko hayo.

No comments: