Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, February 24, 2012

Umoja wa mataifa umesema kuwa idadi ya watu wanaokimbia maeneo ya Kaskazini mwa taifa la Mali sasa imeongezeka na kufikia watu 20,000.

Takriba watu nusu milioni wamekimbilia mataifa jirani baada ya kundi jipya la waasi wa Tuareg kuanzisha mashambulio dhidi ya vikosi vya serikali wiki iliyopita.
Kwa mujibu wa umoja wa mataifa takriban watu 1000 wanavuka mpaka wa Mali na kuingia katika mataifa jirani kila siku.
Hii inafanya idadi ya watu waliolazimika kuishi maisha ya ukimbizi nchini mwao na wale wanaokimbilia mataifa jirani kufikia takriban watu 125,000.

No comments: