Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, July 1, 2013

Watu wenye silaha washambulia jela huko Nigeria

Shambulio la watu wenye silaha katika jela moja huko kusini mwa Nigeria, limesababisha makumi ya wafungwa kutoweka. Maafisa wa Nigeria wametangaza kuwa, tukio hilo lilitokea jana katika jela moja ya mji wa Akure, kusini mwa nchi hiyo na kuwatorosha wafungwa wapatao 175. Aidha kwa mujibu wa ripoti hiyo, watu 2 waliuawa na wengine kujerihiwa. Habari zaidi zinasema kuwa, kulitumika mabomu na silaha nzito katika shambulio hilo. Hii ni katika hali ambayo katika miezi ya hivi karibuni, wapiganaji wa kundi la Boko Haram wamekuwa wakitekeleza mashambulizi katika jela kadhaa katika miji mbalimbali ya Nigeria.
Kabla ya hapo pia maafisa wa jeshi la nchi hiyo, walitangaza kuawa watu 22 wakiwemo polisi wawili na wapiganaji wa Boko Haram wapatao 20 huko mjini Maiduguri katika mkoa wa Borno nchini humo. Terehe 14 Mei mwaka huu, Rais Goodluck Jonathan wa Nigeria alitangaza hali ya hatari katika majimbo ya Borno, Yobe na Adamawa, baada ya wapiganaji wa Boko Haram kutangaza vita dhidi ya serikali yake.

No comments: