Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, July 1, 2013

Wapinzani nchini Algeria wataka uchaguzi wa Rais

Vyama na makundi ya kisiasa yanayoipinga serikali ya Algeria vimetaka kufanyika uchaguzi wa kabla ya wakati kwa mujibu wa katiba kutokana na kuugua rais wa nchi hiyo. Vyama vingi vya upinzania vinataka kufanyika uchaguzi wa kabla ya wakati huko Algeria na kutangazwa rais mpya atayechukua majukumu ya kuiongoza nchi. Jahid Yonus Katibu Mkuu wa Harakati ya Kitaifa ya Marekebisho ya Algeria amesema kuwa vyama na makundi ya kisiasa nchini humo yanapasa kufikia makubaliano na kumchagua mgombea mmoja atakayeshiriki katika uchaguzi ujao wa rais.
Katibu Mkuu wa Harakati ya Kitaifa ya Marekebisho ya Algeria amekosoa utendaji wa kisiasa wa baadhi ya viongozi wa serikali na kutahadharisha kuwa, mfumo wa uongozi wa Algeria unaelekea upande wa mfumo wa kifalme. Jahid Yunisi ameongeza kuwa, viongozi wa serikali ya Algeria wanadhibiti vyombo vya habari ili kupotosha fikra za walio wengi nchini humo. Rais Abdulaziz Butafliqa wa Algeria hivi sasa amelazwa hospitalini nchini Ufaransa baada kupatwa na kiharusi siku kadhaa zilizopita.

No comments: