Watu wasiopungua wanane wamejeruhiwa baada mwanaume mmoja kufaytua
risasi katika eneo la makazi ya raia huko Brooklyn mjini New York,
Marekani. Ufyatuaji risasi huo umetokea leo asubuhi huko East Flatbush.
Wanaume wanne na wanawake wanne ni miongoni mwa majeruhi ambao
walikimbizwa katika hospitali za karibu baada ya tukio hilo. Mtu mmoja
kati ya hao amejeruhiwa vibaya sana na hali yake imeripotiwa kuwa mbaya.
Hadi sasa hakuna mtu yoyote aliyetiwa nguvuni kuhusiana na ufyatuaji
risasi huo uliofanywa mapema leo asubuhi.
Ufyatuaji risasi ulitokea leo
huko Brooklyn umejiri ikiwa zimepita siku chache tu baada ya watu
wengine saba kuuawa na wengine 29 kujeruhiwa katika tukio kama hilo huko
Chicago. Takwimu za FBI zinaonyesha kuwa watu 8583 waliuliwa kwa risasi
nchini Marekani mwaka juzi, kiwango ambacho ni sawa na kuuawa watu 24
kwa siku.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment