Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, July 1, 2013

Abd Rabbuh Mansur: Saleh asiingile mambo ya nchi

Rais Abd Rabbuh Mansur Hadi wa Yemen amemtaka rais aliyeenguliwa madarakani Ali Abdullah Saleh, kuacha kuingilia mambo ya ndani ya nchi hiyo. Rais Abd Rabbuh Mansur amekosoa vikali matamshi ya Saleh dikteta wa zamani wa Yemen aliyesema kuwa, hivi sasa nchi hiyo haina amani na utulivu na kuongeza kuwa, ikiwa dikteta huyo hatoacha mwenendo wake huo, basi atafichua faili la ufisadi mkubwa wa viongozi wa utawala wake uliopita.
Aidha Saleh sambamba na kukosoa serikali ya sasa ya Abd Rabbuh Mansur Hadi kuwa haina uwezo wa kuongoza, ameituhumu pia kwa kushindwa kurejesha amani na utulivu nchini. Rais Abd Rabbuh Mansur alishika hatamu za uongozi wa Yemen kutoka kwa Ali Abdullah Saleh mnamo tarehe 21 Februari mwaka 2012 kwa mujibu wa makubaliano ya kukabidhi madaraka, yaliyofanyika kwa mpango wa Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi. Hivi sasa rais huyo anakabiliwa na changamoto nyingi hususan madai ya kujitenga kusini mwa nchi hiyo, kuendelea kupenyeza serikalini wafuasi wa Saleh na kukosekana usalama kunakosababishwa na kuwepo wanamgambo wa Al-Qaida nchini humo.

No comments: