Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Sunday, June 1, 2014

Upinzani Bahrain kususia uchaguzi wa Oktoba

Vyama vya upinzani vya Bahrain vimesema kuwa vitasusia uchaguzi wa bunge na mabaraza ya miji, uliopangwa kufanyika mwezi Oktoba. Taarifa iliyotolewa na vyama hivyo imesema kuwa, havitoshiriki katika uchaguzi huo bila ya kufikiwa makubaliano ya wazi ya kisiasa yanayoakisi matakwa ya wananchi.
Tarifa hiyo iliyotolewa baada ya kufanyika mkutano katika makao makuu ya mrengo wa upinzani wa al Wefaq imeeleza kwamba, uchaguzi huo unapasa kuchagua serikali iliyoteuliwa kwa mujibu wa matakwa ya wananchi na kwamba upinzani utaendelea na harakati za amani za kupigania demokrasia.
Tangu mwaka 2011 maelfu ya wananchi wanaotaka demokrasia na mageuzi nchini Bahrain wamekuwa wakiandamana nchini humo, wakitaka utawala wa kifalme wa Aal Khalifa uondoke madarakani. Waandamanaji hao wamekuwa wakikandamizwa na vikosi vya usalama na kutiwa mbaroni.

No comments: