Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Sunday, June 1, 2014

Machar hawezi kuwadhibiti waasi Sudan Kusini

Riek Machar kiongozi wa waasi wa Sudan Kusini na makamu wa rais wa zamani amesema kuwa, hana udhibiti kamili wa vikosi vya waasi ambavyo vinatuhumiwa kuleta machafuko nchini humo.  Akihojiwa na shirika la habari la AFP mjini Nairobi nchini Kenya, Machar ameeleza kwamba, itakuwa si kweli akisema kuwa anawadhibiti waasi wote lakini kwamba ana matumaini ataweza kuwadhibiti kwani wamewapa mafunzo na miongozo.
Kiongozi huyo wa waasi wa Sudan Kusini aidha amesema, katika jeshi lao kuna wapiganaji waliojitolea, ambao wana silaha zao wenyewe na wamejiunga kwenye vita.
Mapigano yaliyojiri kati ya jeshi la Sudan Kusini na waasi watiifu kwa Rieck Machar yamesababisha maelfu ya watu kupoteza maisha na wengine zaidi ya milioni 1.3 kuwa wakimbizi.  Makubaliano ya kusitisha mapigano yalifikiwa hivi karibuni kati ya pande hizo mbili huku mazungumzo ya kusaka amani ya kudumu yakiendelea.

No comments: