Serikali ya Ethiopia imepuuza malalamiko yanayotolewa na serikali ya
Misri na imesisitiza juu ya kuendelea na ujenzi wa bwawa la an Nahdha.
Msemaji wa Waziri Mkuu wa Ethiopia amesema kuwa, malalamiko yanayotolewa
na Misri ya kuitaka Ethiopia isitishe ujenzi wa bwawa hilo
hayakubaliki. Hayo yanaelezwa katika hali ambayo, Essam Haddad mshauri
wa masuala ya kigeni wa Rais Muhammad Morsi wa Misri amesema kuwa,
Cairo haitatumia njia za kijeshi kwa lengo la kuukwamua mgogoro wa
bwawa la an Nahdha. Imeelezwa kuwa, ujenzi wa bwawa hilo utasababisha
kupungua hisa ya Misri ya karibu cubic miter bilioni 55 na milioni 500
ya maji kila mwaka, kwa mujibu wa makubaliano ya kimataifa yaliyotiwa
saini mwaka 1929 na 1959. Wataalamu wa masuala ya kilimo wanasema kuwa,
hatua ya ghafla ya Ethiopia ya kuweka mkondo mpya wa maji ya Mto Nile
na yatakayoelekea kwenye bwawa hilo, utasababisha athari kubwa katika
sekta ya kilimo katika nchi za Misri na Sudan.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)







No comments:
Post a Comment