![]() |
| Sergei Lavrog - Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia |
Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia imesema Moscow itapinga azimio
linalotarajiwa kuwasilishwa mbele ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa
dhidi ya Syria. Taarifa ya wizara ya Mambo ya Nje ya Russia imesema
kuwa, rasimu ya azimio hilo inaonyesha mambo mengi ya uongo kuhusu
kadhia ya Syria. Taarifa hiyo imefafanua kwamba azimio hilo linaituhumu
serikali ya Rais Bashar Asad kuwa ndiyo yenye kusababisha mauaji na
ghasia bila ya kutaja nafasi ya makundi ya kigaidi katika mgogoro huo.
Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia imehoji ni kwa nini azimio hilo
halizungumzii jinsi magaidi wa Syria wanavyowaua raia wa kawaida kila
siku.
Russia pia imesema azimio hilo linalenga kupindua serikali halali
ya Syria iliyochaguliwa kwa njia ya kidemokrasia. Tayari Russia imepinga
maazimio mawili dhidi ya Syria katika Baraza la Usalama la Umoja wa
Mataifa katika siku za huko nyuma.






No comments:
Post a Comment