Miaka 19 iliyopita na katika siku kama ya leo, nchi ya Eritrea iliyoko kaskazini mashariki mwa bara la Afrika ilipata uhuru kutoka kwa Ethiopia. Mwaka 1936 Italia iliikalia kwa mabavu Eritrea iliyokuwa ikihesabiwa katika zama hizo kuwa ni sehemu ya ardhi ya Ethiopia. Mwaka 1953, Italia iliirejeshea Ethiopia ardhi hiyo. Hata hivyo wananchi wengi wa nchi hiyo waliokuwa wakitaka uhuru walianzisha harakati za ukombozi dhidi ya serikali ya Ethiopia. Mwaka 1991, Harakati ya Ukombozi wa Eritrea ikisaidiana na wanamapinduzi wa Ethiopia walihitimisha utawala wa kidikteta wa Mengistu Haile Mariam, na wakakubaliana kuanishwa mustakbali wa Eritrea mwaka 1993 kwa kura ya maoni. Washiriki wengi wa kura hiyo ya maoni walipiga kura ya kutaka kujitawala Eritrea. ***
Na siku kama ya leo miaka 993 iliyopita, aliaga dunia Abu Rayhan Biruni msomi stadi na mahiri wa Kiirani. Tangu anaanza kusoma, Abu Rayhan Biruni alikuwa na mapenzi makubwa na maalumu na elimu ya hisabati. Hima na bidii yake ilifanya muda si mrefu ajitokeze na kuwa mwalimu mkubwa katika elimu ya hisabati.






No comments:
Post a Comment