Idara ya kupambana na ugaidi nchini Iraq imethibitisha kuuawa mufti wa
kundi la Dola la Kiislamu la Iraq na Sham kwa kifupi Daesh huko mjini
Tikrit nchini humo. Kwa mujibu wa idara hiyo, mufti huyo wa kundi hilo
la kigaidi Swaqru an-Naswir, aliuawa katika operesheni ya jeshi la Iraq
iliyofanikiwa katika mji huo. Habari zinasema kuwa, operesheni hiyo
ilifanyika kwa kutegemea habari za kiintelijensia katika mji huo. Katika
operesheni hizo, zaidi ya wanamgambo 150 wa kundi hilo wameuawa na
kujeruhiwa mjini hapo.
Jeshi la Iraq kwa kutumia ndege za kivita jana
lilililenga mkusanyiko mkubwa wa magaidi hao na kuua wengi kati yao.
Aidha jeshi la Iraq hapo jana pia lilifanikiwa kuuangamiza msafara wa
magari ya kundi hilo yapatayo 200 uliokuwa ukielekea mji wa Samarra. Hii
ni katika hali ambayo, Nour al Maliki Waziri Mkuu wa Iraq amelipa amri
jeshi la nchi hiyo kuisafisha miji yote ya Iraq kutokana na uepo wa
kundi la Daesh. Kwengineko sheikh mkubwa wa Kisuni amelitaja kundi la
Daesh kuwa ni kundi lililopotea na kwamba halina uhusiano wowote na
dhehebu la Kisuni. Sheikh Muhammad Amin mmoja wa wajumbe wa Jumuiya ya
Maulama wa Iraq ameyasema hayo kupitia kanali ya televisheni ya Sumaria
News na kusema kuwa, hii leo Iraq inakabiliwa na hujuma za matakfiri
ambao wanatekeleza ajenda za mabwana zao kwa lengo la kuigeuza Iraq kuwa
kichaka cha ugaidi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)







No comments:
Post a Comment