Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, July 17, 2013

Ikhwan: Kumrejesha Mursi ndilo suala muhimu Misri

Makamu Mwenyekiti wa chama cha Uhuru na Uadilifu tawi la kisiasa la Ikhwanul Muslimiin nchini Misri amesema kuwa, suala muhimu hivi sasa ni kuondolewa utawala mikononi mwa jeshi kurejewshwa serikali ya kisheria nchini humo. Issam al-Iryan ameweka wazi kuwa, Ikhwanul Muslimiin haipingi kufanya kazi zake chini ya katiba na kwamba hadi sasa haijawahi kukiuka sheria yoyote.
Amesema kuwa, hivi sasa juhudi inayofanyika ni kumrejesha madarakani Muhammad Mursi rais aliyeondolewa madarakani ili kuweza kurejesha mwenendo wa demokrasia Misri. Aidha akijibu swali kuhusu safari ya William Joseph Burns Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani mjini Cairo, Misri, al-Iryan amesema kuwa kutokana na hatua ya jeshi kuvunja bunge, kusimamisha utekelezwaji katiba na kuondolewa madarakani rais aliyechaguliwa kisheria nchini humo, hawezi kuwa na imani kwa Rais Barack Obama wa Marekani wala William Burns. Wakati huo huo, Ahmed El-Muslimani mshauri wa rais wa mpito katika masuala ya habari nchini Misri, ameyataka makundi yote ya kisiasa kwa ajili ya maridhiano ya kitaifa.

No comments: