Watu wasiopungua 27 wamejeruhiwa katika mapigano baina ya wafuasi na wapinzani wa rais Mohammad Morsi wa Misri.
Machafuko hayo ya Jumatano katika mkoa wa Fayoum yaliibuka baada ya
mkutano ulioitishwa na harakati ya Ikwanul Muslimin kumuunga mkono Rais
Morsi.
Machafuko yaliibuka pia katika eneo la Nile Delta baada ya rais Morsi
kuwateua wanachama kadhaa wa harakati ya Ikanul Muslimin katika
nyadhifa muhimu serikalini.
Hivi karibuni Rais Morsi aliwateua magavana
wapya ambao wote ni wanachama wa Ikanul Muslimin. Hii inamaanisha kuwa
magavana 11 kati ya 27 kote Misri ni wanachama wa Ikawanul Muslimin.
Weledi wa mambo wanasema Misri inakabiliwa na hitilafu kubwa za
kimitazamo na mgawanyiko wa kijamii na kwamba iwapo masuala hayo mawili
hayatotatuliwa haraka, yanaweza kuwaletea madhara Wamisri wenyewe.







No comments:
Post a Comment