Leo ni Alkhamisi tarehe 11 Shaaban mwaka 1434 Hijria sawa na tarehe 20 Juni 2013 Miladia.
Miaka 1401 iliyopita katika siku kama ya leo mwaka 33 Hijria Qamaria
alizaliwa mjini Madina Ali bin Hussein, mwana mkubwa wa Imam Hussein AS,
Mjukuu wa Mtume Muhamad SAW. Alishabihiana sana na Mtume SAW na
aliweza kunufaika kwa fadhila za maadila meme na maarifa ya Kiislamu
kutoka kwa babu yake, Imam Ali AS na baba yake Imam Hussein AS. Kutokana
na kuwa jina la Ali bin Hussein lilishabihiana sana na jina la ndugu
yake mdogo ambaye pia alijulikana kama Ali, alipewa lakabu ya 'Ali
Akbar' yaani Ali mkubwa. Alikuwa na nafasi kubwa katika harakati na
mwamko wa baba yake mtukufu dhidi ya dhulma na utawala wa kiimala wa
Bani Umayya.
Aliendeleza harakati hizo na katika siku ya tarehe 10
Muharram mwaka 61 Hijria Qamaria, akiwa katika medani ya vita bega kwa
bega na baba yake walipambana na jeshi katili ya Muawiyya huko Karbala
na kwa ushujaa mkubwa aliuawa Shahidi.
@@
Miaka 101 iliyopita msomi wa Poland kwa jina la Casimir Funk kwa mara
ya kwanza kabisa alifanikiwa kugundua vitamin au virutubisho. Baada ya
uhakiki mwingi Daktari Casimir Funk aligundua kwamba vyakula
vinavyotumiwa na mwanadamu vina baadhi ya virutubisho (vitamin) ambavyo
japokuwa ni vichache sana lakini vina udharura mkubwa katika ukuaji na
usalama wa mwili na akaamua kuvipa jina la Vitamini. Kuna anua ya
vitamin kama vile , A,B, C, D, E na K na kila moja ina sifa na kazi
maalumu katika mwili wa mwanaadamu.
@@@
Na siku kama ya leo miaka 40 iliyopita, inayosadifiana na tarehe 20
Juni 1973, Jose Domingo Peron mwanasiasa na muasisi wa Chama cha
Peronist nchini Argentina, alirejea nchini mwake akitokea uhamishoni.
Peron alikuwa afisa katika jeshi na alifanikiwa kuwa Rais wa Argentina
mwaka 1946, na kufanya mabadiliko makubwa nchini humo. Hata hivyo
udikteta wa Jose Domingo ulipunguza wafuasi wake na mwaka 1955
aliondolewa madarakani baada ya kufanyika mapinduzi. Lakini miezi
michache baada ya kurejea kutoka uhamishoni Jose Domingo alifanikiwa
kurejea tena madarakani na kuwa Rais wa Argentina. Mwaka mmoja baada ya
kurejea madarakani Jose Domingo alifariki dunia, na mke wake Isabel
Martines de Peron akawa Rais wa Argentina kuanzia mwaka 1974 hadi 1976.







No comments:
Post a Comment