Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Thursday, January 24, 2013

Iran yataka vita visitishwe nchini Mali

Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imeitaka Ufaransa isitishe vita inavyoongoza dhidi ya Mali.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran anayeshughulikia masuala ya nchi za Kiafrika na Kiarabu Hossein Amir-Abdollahian ametoa wito huo siku ya Jumatano huku akisisitiza kuwa mipaka na umoja wa Mali unapaswa kulindwa.
Ameongeza kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inafuatilia kwa karibu matukio ya Mali na kwamba  inasikitika kuona mauaji  na kuachwa bila makao maelfu ya raia wa nchi hiyo. Abdollahian amesema Iran ambayo ni mwenyekiti wa mzunguko wa Harakati ya Nchi Zisizofungamana na Siasa za Upande Wowote NAM iko tayari kurejesha amani na umoja wa mipaka ya Mali.
Januari 11 Ufaransa ilianzisha vita nchini Mali kwa kisingizio cha kukabiliana na wanamgambo wa eneo la kaskazini mwa nchi hiyo ya Magharibi mwa Afrika.

No comments: