Katika upande mwengine Alaauddin Bourujerdi, Mkuu wa Kamisheni ya Usalama wa Taifa na Siasa za Nje katika Bunge la Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu inaitambua Bahrain kama nchi huru na mwanachama wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu OIC, na kwa sababu hiyo inapinga hatua ya Saudi Arabia na nchi nyengine ya kuingilia masuala ya ndani ya Bahrain ambayo ni nchi huru inayojitawala. Wakati huohuo kanali ya televisheni ya al Manar ya Lebanon imetangaza kuwa mpango wa kutaka kuiunganisha Bahrain na Saudia unalenga kuzuia wimbi la mapinduzi kutoka nchi moja hadi nyengine na kutibuka hali ya mambo katika Mashariki ya Kati. Ripoti ya kanali hiyo imeongeza kuwa kutokana na wimbi la mwamko wa Kiislamu na mapambano ya wananchi wa mataifa ya Kiislamu katika eneo la Mashariki ya Kati na nchi nyengine zilizoko chini ya tawala za kidhalimu na watawala waovu na mafisadi hususan nchini Bahrain, sambamba na kuingia hatarini maslahi haramu ya Uistikbari wa dunia, katika hali ya kuhaha na kutapatapa, madola ya kidhalimu yamezidi kuchukua ili maslahi yao haramu yasiingie hatarini zaidi. Kwa mujibu wa al Manar njama hatari ya kutaka kuiunganisha Bahrain na Saudi Arabia ni matokeo ya mpango uliobuniwa na mihimili mitatu ya Uistikbaari wa dunia yaani Marekani, Uingereza na utawala wa Kizayuni wa Israel.
Friday, May 25, 2012
Kuendelea upinzani wa wananchi wa Bahrain dhidi ya mpango wa kuunganishwa nchi yao na Saudi Arabia
Katika upande mwengine Alaauddin Bourujerdi, Mkuu wa Kamisheni ya Usalama wa Taifa na Siasa za Nje katika Bunge la Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu inaitambua Bahrain kama nchi huru na mwanachama wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu OIC, na kwa sababu hiyo inapinga hatua ya Saudi Arabia na nchi nyengine ya kuingilia masuala ya ndani ya Bahrain ambayo ni nchi huru inayojitawala. Wakati huohuo kanali ya televisheni ya al Manar ya Lebanon imetangaza kuwa mpango wa kutaka kuiunganisha Bahrain na Saudia unalenga kuzuia wimbi la mapinduzi kutoka nchi moja hadi nyengine na kutibuka hali ya mambo katika Mashariki ya Kati. Ripoti ya kanali hiyo imeongeza kuwa kutokana na wimbi la mwamko wa Kiislamu na mapambano ya wananchi wa mataifa ya Kiislamu katika eneo la Mashariki ya Kati na nchi nyengine zilizoko chini ya tawala za kidhalimu na watawala waovu na mafisadi hususan nchini Bahrain, sambamba na kuingia hatarini maslahi haramu ya Uistikbari wa dunia, katika hali ya kuhaha na kutapatapa, madola ya kidhalimu yamezidi kuchukua ili maslahi yao haramu yasiingie hatarini zaidi. Kwa mujibu wa al Manar njama hatari ya kutaka kuiunganisha Bahrain na Saudi Arabia ni matokeo ya mpango uliobuniwa na mihimili mitatu ya Uistikbaari wa dunia yaani Marekani, Uingereza na utawala wa Kizayuni wa Israel.
Posted by
AO Secretarial & Technology Supplies
Labels:
Kuendelea upinzani wa wananchi wa Bahrain dhidi ya mpango wa kuunganishwa nchi yao na Saudi Arabia
Subscribe to:
Post Comments (Atom)






No comments:
Post a Comment