Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Thursday, March 1, 2012

Ndege za Marekani zahujumu Somalia na kuua watu kadhaa


Watu kadhaa wameuawa baada ya ndege zisizo na rubani za Marekani kushambulia kwa makombora maeneo ya nje ya mji mkuu wa Somalia Mogadishu.Hujuma hiyo Jumanne usiku ya ndege za kigaidi za Marekani zisizo na rubani imelenga maeneo kadhaa kusini mwa Mogadishu. Wakati huo huo ndege moja isiyo na rubani ya Marekani imeanguka karibu na kituo cha kijeshi cha Halane kusini mwa Mogadishu.Maafisa wa Somalia wamethibitisha kuwa ndege hiyo ya kijasusi ilianguka siku ya Jumatano.
Oktoba 28 mwaka jana Marekani ilikiri kushambulia Somalia kwa ndege zake hizo kutumia kituo cha kijeshi cha siri kilichoko Ethiopia, eti kwa lengo la kukabiliana na waasi wa as Shabab.
Hata hivyo raia na watu wa kawaida Somalia ndio wahanga wakuu wa mashambulizi ya ndege za kigaidi za Marekani nchini humo.
www.kiswahili.irib.ir

No comments: