Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, May 31, 2014

AI yakosoa kunyanyaswa kijinsia wanawake India

Shirika la Msamaha Duniani Amnesty International limewakosoa maafisa wa India kutokana na ubaguzi na unyanyasaji wa kijinsia dhidi ya wanawake na wasichana unaoshuhudiwa nchini humo.  Shirika hilo limeitaka serikali ya India kuchukua hatua za haraka za kulinda haki za wanawake na kuacha kuwasamehe wanaotenda jinai hizo.
Pia Amnesty International imewataka maafisa wa India kuchunguza bila upendeleo tukio la hivi karibuni la kubakwa na kuuawa wasichana wawili katika kijiji cha jimbo la kaskazini la Uttar Pradesh.
Ripoti zinasema kuwa, katika kila dakika 22 mwanamke mmoja hubakwa nchini India. Mwaka jana serikali ya nchi hiyo ilitangaza adhabu ya kifo kwa watakaobaka kwa pamoja hata kama atakayebakwa atabakia hai. Adhabu hiyo ilitangazwa, baada ya msichana wa chuo kikuu aliyekuwa na miaka 23 kubakwa na kundi la wanaume na kisha kurushwa nje ya basi katika tukio la kinyama lililofanywa katika mji mkuu New Delhi mwaka 2012.

No comments: