Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, June 21, 2013

Mtuhumiwa wa mauaji Rwanda afungwa Sweden

Mahakama ya Stockholm nchini Sweden imemuhukumu adhabu ya kifungo cha maisha jela Stanislas Mbanenande Mswidi mwenye asili ya Rwanda baada ya kupatikana na hatia ya kushiriki kwenye mauaji ya kimbari nchini Rwanda. Mahakama hiyo imeeleza, Mbanenande akishirikiana na watu wengine alitenda jinai  za mauaji ya halaiki nchini humo katika eneo la Kibuye magharibi mwa Rwanda kuanzia tarehe 6 Aprili hadi 30 Juni mwaka 1994. Hata hivyo, wakati wa kusikilizwa kesi hiyo, Stanislas alikadhibisha tuhuma hizo zilizoelekezwa dhidi yake.
Mashuhuda kadhaa wameeleza mahakamani hapo kwamba, Mbanenande alishiriki kikamilifu kwenye vitendo vya mauaji na hasa kwenye kanisa moja na uwanja wa michezo nchini Rwanda. Inafaa kuashiria hapa kuwa, Stanislas Mbanenande alikimbilia nchini Sweden mwaka 2007, na mwaka uliofuata alipata uraia wa nchi hiyo. Imeelezwa kuwa, watu wasiopungua laki nane waliuawa kwenye machafuko ya Rwanda mwaka 1994.

No comments: