Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, May 26, 2012

Kikosi cha AMISOM chadhibiti mji muhimu nchini Somalia


Kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Afrika nchini Somalia AMISOM kikishirikiana na askari wa serikali ya nchi hiyo kimeudhibiti mji wa Afgoye uliokuwa ukitumiwa kama ngome ya wanamgambo wa ash Shabab nchini humo.
Hatua hiyo inahesabiwa kuwa pigo kubwa kwa wanamgambo hao waliokuwa wakitumia mji huo kushambulia mji mkuu Mogadishu.
Paddy Ankunda, msemaji wa kikosi cha AMISON amesema kwamba, wamevuuka mto Shabelle na hivi sasa wako katika mji wa Afgoye ambao tayari wanaudhibiti. Amesema, wamekuwa wakipigana tangu Jumanne na hivi sasa wamefanikiwa kufikia lengo walilokusudia.
Ankunda aidha ameongeza kuwa, wapiganaji wa ash Shabab wanaendelea kuukimbia mji huo kuelekea maporini na kwamba vikosi vya AU hivi sasa vimeimarisha usalama katika barabara za kuingia kwenye mji wa Afgoye, ambazo ni njia kuu ya kutoka kusini mwa Somalia kuelekea mji mkuu Mogadishu.

No comments: